Serikali ya Burkina Faso imetangaza kuongeza hatua za kiusalama katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo kufuatia mashambulizi ya hivi karibuni nchini jirani Mali.
Hatua hiyo imechukuliwa kutokana na hofu ya kusambaa kwa vitendo vya vurugu mpakani, hasa ikizingatiwa kuwa nchi hizo mbili zinashirikiana katika kanda ya Sahel ambayo imekuwa ikikabiliwa na changamoto za usalama kwa muda mrefu,
Mamlaka zimeongeza doria za kijeshi, kuweka vizuizi katika barabara kuu na kuimarisha ulinzi katika maeneo nyeti kama mipaka, masoko na vituo vya usafiri,
Serikali pia imewataka wananchi kuwa waangalifu na kuripoti harakati zozote zinazotiliwa shaka, huku ikisisitiza kuwa hatua hizo ni za tahadhari ili kuzuia mashambulizi yanayoweza kutokea.
Wachambuzi wa usalama wanasema kuwa hatua hiyo inaonyesha wasiwasi mkubwa kuhusu kuenea kwa makundi yenye silaha katika eneo la Sahel, ambapo nchi nyingi zinaendelea kupambana na vitisho vya ugaidi.
Chanzo:Africanews
















