Wakati Afrika ikiendelea kuongeza kasi ya matumizi ya nishati jadidifu, hasa nishati ya jua, wataalamu wameonya kuhusu hatari inayoongezeka ya kiafya inayotokana na ongezeko la urejelezaji wa betri za lead katika mazingira yasiyo salama.
Kwa mujibu wa wachunguzi, mahitaji makubwa ya betri yanayosababishwa na mifumo ya umeme wa jua nje ya gridi yameongeza shughuli za urejelezaji, hasa katika sekta isiyo rasmi ambayo haina udhibiti wa kutosha.
Hali hii imeibua hofu ya kuongezeka kwa sumu ya risasi, tatizo linaloweza kusababisha madhara makubwa kwa afya ya jamii na uchumi wa bara zima.
CHANZO: TRT Afrika
















