Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza kuwa operesheni kubwa ya kijeshi iliyoendeshwa na Marekani imesababisha kuondolewa kwa Rais wa Venezuela, Nicolás Maduro, pamoja na mkewe kutoka nchini humo.
Kupitia taarifa aliyochapisha Jumamosi kwenye mtandao wake wa kijamii wa Truth Social, Trump alisema kuwa Marekani ilifanikiwa kutekeleza shambulio la kina dhidi ya uongozi wa Venezuela, hatua iliyosababisha kukamatwa kwa Maduro na mkewe kabla ya kuhamishwa nje ya nchi.
Trump alieleza kuwa operesheni hiyo ilifanyika kwa ushirikiano wa karibu kati ya vikosi vya kijeshi na vyombo vya utekelezaji wa sheria vya Marekani, akisisitiza kuwa hatua hiyo ilikuwa sehemu ya mkakati mpana wa kushughulikia hali ya kisiasa nchini Venezuela.
CHANZO: TRT Afrika














