Umoja wa Afrika ulihimiza viongozi wenye busara kuonyesha utulivu na subira siku ya Jumamosi baada ya Marekani na Israel kufanya mashambulizi dhidi ya Iran, na kuonya kwamba migogoro inaweza kuhatarisha zaidi maisha ya watu katika kanda hilo.
Mkuu wa shirika hilo barani Afrika, Mahamoud Ali Youssouf alitoa wito wa “kujizuia, na kurejelewa mazungumzo endelevu”.
“Kuongezeka uhasama zaidi kunahatarisha kudorora kwa usalama na utulivu duniani, kukiwa na athari kubwa kwa masoko ya nishati, usalama wa chakula, na ustahimilivu wa kiuchumi hasa katika Afrika, ambako migogoro na shinikizo la kiuchumi bado ni kubwa.”
Chanzo: TRT Afrika














